East Coast Team kuingia kambini kuandaa ngoma mpya, maproducer wanne kuhusika!

East Coast Team inarejea tena. King Crazy GK, AY, Mwana FA, Snare na Buff G, wanatarajia kuingia kambini hivi karibuni kuandaa nyimbo mpya. Maproducer wanne watashiriki kwenye mradi huo.


Wasanii wa East Coast AY, GK, Snare pamoja na Buff G

GK ameimbia Bongo5 kuwa wapo kwenye maandalizi ya mwisho kuingia kambini na kuanza kazi hiyo.

“Tumechagua ma-producer wanne, tumemchagua Marco Chali, tumemchangua John Maundi, Mr T Touch na kuna mwingine mmoja. Producer wote watatengeneza halafu tutachagua,” amesema GK. “Hii ni project ya East Coast. Kuna kwenda nje kufanya video lakini tunataka kwenda speed. Leo tunakaa tena kupanga. Tumeshachukua kabisa nyumba sehemu ya vyumba kadhaa tutakaa mule tutajiandaa. Kuna vitu vingi vitaendelea hapo. Unajua toka East Coast imetoka ilikuwa inafanya muziki fulani tofauti lakini ni Hip Hop, aina fulani hivi ambayo ndio maana umeona watu wameendelea kumiss na wanatuona tunachelewa.”

0 comments:

Post a Comment

Recent Posts