NASRI: RIBERY ANASTAHILI KUWA MCHEZAJI BORA WA DUNIA

Franck Ribery
Upepo wa mchezaji bora wa dunia unadizi kuelekea kwa mchezaji wa kimataifa Franck Ribery baada ya wadau mbalimbali wa soka duniani kumpigia upatu mkali huyo kutoka Bayern Munich.
Kiungo wa Manchestar City, Samir Nasri  naye amejitokeza na kumfagilia mchezaji mwenzie wa timu ya taifa ya Ufaransa kuwa anastaili kuwa mhezaji bora wa dunia.
"ribery alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa ulaya hivyo nina matuamini makubwa kuwa atashinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia.
Ribery amekuwa na wakati mgumu katika timu yake ya taifa kutokana na kutokuwa na mchango mkubwa katika timu yake ya taifa ukilinganisha na klabu yake ya kulipwa ambapo amekuwa lulu na kutegemewa sana.
Taji la mchezaji bora wa dunia linashikiliwa na Lionel Messi ambaye ameshinda taji hilo mara tatu mfulullizo

0 comments:

Post a Comment

Recent Posts