Asha Mandela: Mwanamke mwenye rasta ndefu zaidi duniani, ni za futi 55
Pamoja na kuonywa na madaktari kuwa urefu wa nywele zake unaweza kumsababishia tatizo la kupooza, Asha Mandela amesema hawezi kuzikata. Mama huyo mwenye mtoto mmoja aishiye Atlanta, Georgia amesema: Nywele zangu zimekuwa sehemu yangu. Ni maisha yangu. Sitozikata kamwe. Kuzikata itakuwa ni
kama kujiua. Itakuwa ni sawa na zombie.’ Mrs Mandela, 47, anashikilia Guinness World Record kwa kuwa na rasta ndefu zaidi duniani zenye urefu wa futi 55. Humchukua siku mbili kuziosha na kuzikausha nywele zake. Mrs Mandela, ana mtoto mwenye miaka 11 aitwaye Zion aliyezaa na mume wake wa pili, anasema nywele zake zimesaidia uhusiano wake na mumewe. Kwa sasa ameolewa na mume wa tatu na asili yake ni Trinidad and Tobago. Alianza kuzitunza nywele hizo miaka 25 iliyopita.
You may also Like
Followers
Tags 2
Popular Posts
-
He Yide (5) ambaye amepewa jina la utani la Duoduo mkazi wa Nanjing China ameweka rekodi ya kuwa rubani mdogo zaidi duniani na sijui kama ...
-
Je utawezaje kutambua fursa na kuweza kuanzisha biashara katika mazingira yako? Bila shaka hili swali watu wengi wanaotamani kumiliki bias...