LYRICS: Stamina Ft. Walter Chilambo - Mguu Pande Mguu Sawa

Song: mguu pande mguu sawa

Artist: stamina ft walter chilambo

Studio: one love fx

Producer; tiddy hotter

Song writer: stamina (verse),walter (choruss)



Intro;stamina

Yeaaah,,,u know what tiddy

One love fx again men

Iz moro town in da house

Shorwebwenzi on this one


Vers 1(stamina)

Peleka kitanda batani,kama unapenda ukeshe bar/

Sista duu muda hausimami,hata uivulie nguo saa/

Ishi kiushujaa,kama umepanga kambi ya jeshi/

Kati ya maarufu na star,maarufu anaongoza kwa deshi/

Ewe raisi wa wanyama,fanya sensa usisahau/

Mfuasi aliyesaliti chama,huku mjini bonge la nyau/

Tunza bible sio irizi,ufalme wa mbingu hauna fensi/

Ndo maana akifaga mzinzi,mazishi hatufanyi gesti/

Chagua kilicho best,kati ya copy na kupaste/

Je Yule aliyefeli maisha na class alifeli test?/

Hakuna demu anayejiuza,hicho ndo nikijuacho/

Nachojua wanakodisha,unatumia huondoki nacho/

Bitozi msaka mchumba,usiforce unapotemwa/

Piga goti kwa muumba,ikibidi akuumbe tena/

Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/

Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/


Chorus(walter chilambo)

Naamini kama nyuma ulikosea rudi

Weka mambo sawa na plan b

Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)

Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)

Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2

Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)

Nyuma geukaaaaaa.


Verse 2(stamina)

Mjini wanyama kibao,cha ajabu wanakula unga/

Mawazo ya vichwa vyao,dingi afe warithi nyumba/

Ewe kengeza,chunga usimcheke chongo/

Cha msingi muombe ebeneza,akupe vision yenye michongo/

Saka chaka kila sehemu,maana pesa ina machale/

Nyie mnaowinda mademu,hivi mna nyota ya mshale?/

Mnyamazie mshenzi,ukimjibu tu anatuna/

Hadi shoga nae ana mpenzi?,kweli madem mna huruma/

Mziki umejaa stress,ambazo haziishagi kwa pombe/

Mastar wamewekeza desi,wanakufa hawana hata ng’ombe/

Underground chondechonde,usiache shule kisa mziki/

Usuperstar una mabonde,na miteremko ya dhiki/

Yesu anarudi lini?,hilo swali ndo ujiulize/

Sio stamina utaoa lini,nitajibu tu niko bize/

Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/

Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/


Chorus(walter chilambo)

Naamini kama nyuma ulikosea rudi

Weka mambo sawa na plan b

Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)

Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)

Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2

Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)

Nyuma geukaaaaaa.


Verse 3(stamina)

Usitupe mayai kiholela,zalisha ili uache chata/

Maisha baiskeli ya delela,ukiinama chako unapata/

Kumpa kibogoyo mnofu,kisa nyama bei aghali/

Ni sawa na kumteta kipofu,huku kifikra anaona mbali/

Hakuna zali la mentali,kwenye sayari ya kupendwa/

Mlevi mnywa safari,je unajua unapokwenda?/

Acha mashauzi,sista duu genge linalipa/

Ujanja sio kwenda south,au china ili ukawe striper/

Mapenzi ni kutendwa,mpendaji jiamini/

Sharo ukiona unapendwa,ujue una nyota ya ukimwi/

Ni sawa na uote,usiku una kiss na jini/

Halafu uamke ujikute,una lips stick kwenye ulimi/

Unahitaji akili,sio mashavu yenye dimpoz/

Mwanaume jasiri,hajichubui kisa ana pimpoz/

Mguu mmoja pande,mwingine urudishe sawa/

Hiyo ndo ishara ya kiafande,ya kuweka mambo sawa/


Chorus(walter chilambo)

Naamini kama nyuma ulikosea rudi

Weka mambo sawa na plan b

Unaweza fanya bora zaidi (muda bado)

Mguu pande(mojaaaaa)mguu sawa(mojaaaaa)

Nyuma geuka(moja mbili tatu mojaaa)…..x2

Mguu pandeeee(mojaaaaaa)mguu sawa(mojaaaa)

Nyuma geukaaaaaa.

Bonyeza HAPA ku download wimbo huu

0 comments:

Post a Comment

Recent Posts