Udakuzi: Obama azidi kubanwa na Merkel

Chansela wa Ujerumani Angela Merkel akiwa na Rais Barak Obama wa Marekani
Ufaransa na Ujerumani zimetoa wito wa kufanya makubaliano na Marekani ifikapo mwishoni mwa mwaka huu ili kumaliza tatizo la ujasusi uliofanywa na Marekani .
Hii inafuatia kuwepo kwa taarifa kuwa majajusi wa Marekani walikuwa wakifanya udakuzi wa mawasiliano ya simu ya Chansela wa Ujerumani Angela Merkel pamoja na mamililoni ya raia wa Ufaransa.
Akizungumza katika mkutano wa Jumuiya ya nchi za ulaya Bi Merkel amesama mbegu ya kutoamiana imepandwa na sasa itafanya ushirikiano katika mambo ya kiintelejensia kuwa mgumu.
Wakati huo nyaraka mpya za siri ambazo zimevujishwa na mmarekani Edward Snowden zinaeleza kuwa Marekani imekuwa ikifanya udakuzi wa simu kwa viongozi wa nchi thelathini na tano duniani.
Waraka huo wa siri uliochapishwa kwenye gazeti la the Guardian la Uingereza unaeleza Idara ya Ujasusi ya Marekani ilianza kufuatilia simu hizo baada ya kupewa namba za simu muhimu zipatazo mia mbili kutoka Idara ya Serikali ya Marekani.

0 comments:

Post a Comment

Recent Posts