Forbes Africa & Channel O watoa orodha ya wasanii 10 wa Afrika wanaoingiza mkwanja zaidi


Kwa mara ya kwanza jarida la Forbes Africa limeshirikiana na kituo cha runinga cha Afrika Kusini cha Channel O kupitia kipindi chake cha Top Ten Most kupata orodha ya kwanza na ya uhakika ya wasanii 10 wa Afrika wanaoingiza mkwanja zaidi, Top Ten Mosy Bankable African Artists.
Hata hivyo orodha hiyo imetawaliwa zaidi na wasanii wa Afrika Magharibi.

1. Akon – Senegal
Description: akon-picture-1
Kuwepo kwa Akon kwenye list hii kunaleta utata mkubwa hasa kwakuwa utajiri wake mwingi umetokana na biashara anazozifanya akiwa Marekani, tofauti na wasanii wengine kwenye list ambao pesa zao zote zinatokana na mambo wanayoyafanya barani Afrika. Hiyo ni kama kuwaonea wasanii wenye makazi yao Afrika. Hata hivyo kwa mujibu wa Forbes, utajiri wake unazidi dola milioni 80.
2. Don Jazzy – Nigeria
Description: G14
Utajiri wa Don Jazzy unatokana hasa na madeal ya matangazo na mikataba na makampuni kama Samsung , MTN, Loya Milk na mengine. Mwaka huu alitengeneza wimbo rasmi wa Samsung AFCON2013.Baada ya kuvunjika kwa uhusiano wake na D’Banj na kupelekea kufa kwa Mo’ Hits, producer huyo alifungua record label nyingine, Mavin Records na kusaini wasanii kadhaa akiwemo Tiwa Savage. Pamoja na hivyo pia, Don Jazzy ana miradi kibao kama ya club za starehe, nyumba, kampuni ya nguo na zingine.
3. P-Square
Description: P-Square
Pesa za mapacha hawa zinatokana zaidi na tour zisizo na mwisho. Ni wasanii wanaochaji pesa nyingi zaidi kwa show moja. Mwaka jana walikuwa na ziara kwenye nchi nyingi za Afrika ambako waliingiza mkwanja mrefu kiasi cha kumfanya Peter Okoye anunue nyumba ya kifahari nchini Marekani. Licha ya kuwa na nyumba yao nyingine ya kifahari nchini mwao iitwayo Squareville, wasanii hao wanajenga mjengo mwingine wa hatari ambao unakaribia kumalizika. Deal lao na kampuni ya Glo limewaaingiza karibu shilingi bilioni 1 kila mwaka. Kwa sasa wapo kwenye ziara ya Marekani na Canada.
4. D’Banj
Description: DBanj
Pamoja na kuingiza fedha nyingi kutokana na pesa kubwa anazochaji kwenye show zake (N2.6m kwa show), D’banj hujihusisha pia na biashara kama reality show ya Koko Mansion, Koko Lounge ya Lagos na Uingereza, Koko Foundation na Koko Mobile.
Ameshadaka madeal kibao ya matangazo ikiwa pamoja na mkataba wa naira milioni 30 na kampuni ya Virgin Colours, N25m za Virgin airline, N20m za Nutricima na deal la Globacom, na mkataba wa N100m na UAC. Aliingiza mkwanja mwingine mrefu kwa kushiriki kwenye kampeni ya Rais Goodluck Jonathan. Mwezi June mwaka huu alipata deal nono na kampuni ya Etisalat la N250m.
5. Wizkid
Description: 00
Kukamata namba tano kwa Wizkid ni surprise kwa wengi hasa kwakuwa hana muda mrefu kihivyo kwenye muziki. Wizkid aliingiza dola 350,000 kutokana na deal la Pepsi na pia deal la N50m kutoka kwa MTN. Show anazofanya zinamuingiza fedha nyingi zaidi.Chanzo kingine cha mapato ni mauzo ya nyimbo zake.
6. 2 Face
Description: 2face-idibia
Pamoja na muziki ambapo huchaji dola 500,000 hadi 800,000 kwa show, 2 Face amekuwa akiingiza fedha nyingi kutokana na mikataba ya matangazo kama ya Guinness na Airtel ambayo yote kwa pamoja aliingiza N42m. Ana miliki pia night club. Pia aliingiza N30m za ‘Phat Girlz’. Kwa sasa amewekeza zaidi kwenye biashara ya makazi zinazofikia thamani ya N2.7m

7. Anselmo Ralph

Description: Anselmo Ralph big def_JFvNe
Anselmo Ralph Andrade Lamb ni msanii mkubwa wa Angola. Ni muimbaji R & B, Soul na Kizomba. \
8. Sarkodie
Description: sarkodie-1
Rapper Sarkodie kutoka Ghana ni mjasiriamali mzuri kwani hadi sasa ameshaanzisha miradi kibao ikiwemo simu zake za mkononi, nguo, maji ya kunywa na mingine. Utajiri wake mkubwa umefanya watu wamhisi ni member wa Illuminati.

9. Ice Prince
Description: ice-prince-1024x768
Mwaka huu Ice Prince alikataa deal nono la kampuni ya Glo na kila mmoja akagundua ni kwa kiasi gani rapper huyo ana fedha kiasi cha kukataa deal kama hiyo. Inasemekana alitaka alipwe dola milioni 1. Pesa zake nyingi zimetokana na show anazofanya na pia amekuwa balozi wa One Campaign kwa muda.

10. Banky W
Description: bankywellington
Bankole Wellington mmiliki wa EME records, ndiye aliyemsaidia Wizkid kufika hapo alipo leo. Ameshasaini mikataba ya matangazo na makampuni mengi kama Samsung Electronics West Africa ambao walimlipa $890,000. Banky W alishawahi pia kuwa balozi wa Etisalat na Coca Cola.



Recent Posts